JESHI LA NIGERIA LATANGAZA KUKISHAMBULIA KITUO CHA BOKO HARAM KINACHODAIWA KUTEKA WASICHANA


Jeshi la Nigeria limesema kuwa limekishambulia kituo cha ujasusi cha wapiganaji wa Boko Haram kinachodaiwa kuhusika na utekaji wa wasichana zaidi ya 200 nchini humo.
 
Hata hivyo taarifa za jeshi hilo zinasema kuwa kiongozi wa kituo hicho cha Boko Haram Babuji Ya'ari amekamatwa.
 
Ya'ari pamoja na kutuhumiwa kuhusika katika utekaji wa wasichana hao lakini pia alihusika katika mauaji ya kiongozi wa kijadi wa Gwoza, imebainisha taarifa ya serikali.
 
Jeshi hilo pia limegundua kuwa Ya'ari aliyekuwa mfanya biashara alikuwa akijifanya ni mwanaharakati katika kutokomeza kundi la Boko Haram ili kupata nafasi ya kuchunguza harakati za jeshi la Nigeria na mipango dhidi ya kundi hilo la kigaidi.
 
Anatuhumiwa kuhusika katika maandalizi ya mashambulio kadhaa likiwemo lile lililotokea Maiduguri na makao makuu ya mji wa Borno mwaka 2011


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo