Wanafunzi 1555 wa Msingi na 7457 wa Sekondari Wapata Mimba

Serikali imesema katika kipindi cha mwaka 2021 na 2022 Wanafunzi wa Shule za Msingi waliopata ujauzito ni 1,554 na Sekondari ni 7,457.


Hadi kufikia mwezi January, 2023 Wanafunzi waliorejea Shuleni baada ya kukatiza masomo kwasababu ya ujauzito na kuendelea na masomo ya Elimu ya Sekondari ni 1,692.

Kauli hiyo imetolewa Bungeni leo January 31, 2023 na Naibu Waziri wa Elimu Omary Kipanga wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Hawa Mchafu Chakoma aliyetaka kujua ni Wanafunzi wangapi waliokuwa wajawazito na wangapi wamerejeshwa Shuleni baada ya agizo la Rais.

Aidha Omary Kipanga amesema kwa upande wa Elimu ya Msingi Serikali inaendelea kukusanya taarifa za Wanafunzi waliorejea Shuleni baada ya kukatiza masomo kwa sababu ya ujauzito.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo