Serikali imesema katika kipindi cha mwaka 2021 na 2022 Wanafunzi wa Shule za Msingi waliopata ujauzito ni 1,554 na Sekondari ni 7,457.
Hadi kufikia mwezi January, 2023 Wanafunzi waliorejea Shuleni baada ya kukatiza masomo kwasababu ya ujauzito na kuendelea na masomo ya Elimu ya Sekondari ni 1,692.
Kauli hiyo imetolewa Bungeni leo January 31, 2023 na Naibu Waziri wa Elimu Omary Kipanga wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Hawa Mchafu Chakoma aliyetaka kujua ni Wanafunzi wangapi waliokuwa wajawazito na wangapi wamerejeshwa Shuleni baada ya agizo la Rais.
Aidha Omary Kipanga amesema kwa upande wa Elimu ya Msingi Serikali inaendelea kukusanya taarifa za Wanafunzi waliorejea Shuleni baada ya kukatiza masomo kwa sababu ya ujauzito.